Tulizonazo

Thursday, December 5, 2019

Lionel Messi aibuka tena mshindi wa Ballon d'Or 2019


Messi ndio mshindi wa Ballon d'Or kwa mwaka 2019Haki miliki ya pichaEPA
Image captionMessi ndio mshindi wa Ballon d'Or kwa mwaka 2019
Mshindi wa tuzo ya Ballon d'Or kwa mwaka 2019 si mwingine bali ni Lionel Messi, ambaye amejichukulia kinyang'anyiro cha kuwa mchezaji bora zaidi kwa mara ya sita.
Mchezaji huyo wa Argentina mwenye miaka 32 amenyakua tuzo hiyo baada ya kuikosa toka mwaka 2015 na hii ni kutokana na kuweza kufunga mara 54 katika klabu ya nchini kwake kwa mwaka 2018-19 .
Virgil van Dijk alikuwa mshindi wa pili - yeye ni miongoni mwa wachezaji wanne wa Liverpool katika saba bora, akiwemo Sadio Mane.
Mchezaji wa Juventus Cristiano Ronaldo, aliwahi kutunukiwa tuzo hiyo mara tano na amekuwa watatu katika kura.
Toka mwaka 2008 tuzo hiyo maarufu zaidi ya wasakata kandanda duniani imetawaliwa na washambuliaji hatari katika kizazi cha sasa Messi na Ronaldo.
Mpaka kufikia mwaka 2017, kila mmoja wao akishinda mara tano.
Kiungo wa Real Madrid na timu ya taifa la Croatia Luka Modric aliingilia ufalme wa Messi na Ronaldo baada ya kunyakua tuzo hiyo mwaka jana.
Na sasa Messi amerejea kileleni kwa kumpiku Ronaldo na kuweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kunyakua tuzo hiyo mara sita.
Messi, Ronaldo na Van Dijk
Image captionHii ni mara ya tatu kwa Messi, Ronaldo na Van Dijk kuwania tuzo kwa pamoja mwaka huu.
Hii ilikuwa ni mara ya tatu kwa mwaka huu kwa Messi, Ronaldo na Van Dijk kuwania tuzo moja kwa pamoja.
Mara ya pili wakaminyana katika tuzo za Mchezaji Bora wa Fifa ambapo Messi aliibuka mshindi.
Luka ModricHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMwaka jana, kiungo wa Real Madrid Luka Modric alikuwa mchezaji wa kwanza tofauti na Lionel Messi na Cristiano Ronaldo kushinda tuzo hiyo baada ya miaka 10.
Tano Bora ya Ballon d'Or
1. Leonel Messi (Barcelona na Argentina)
2. Virgil van Dijk (Liverpool na Uholanzi)
3. Cristiano Ronaldo (Juventus na Ureno)
4. Sadio Mane (Liverpool na Senegali)
5. Mohammed Salah (Liverpool na Misri)
Ballon d'Or ni nini?
Tuzo ya Ballon d'Or imekuwa ikitolewa nchini Ufaransa kila mwaka toka 1956, na mshindi wake wa kwanza alikuwa mchezaji kutoka Uingereza Stanley Matthews.
Awali tuzo hiyo ilikuwa ni kwa wachezaji wa Ulaya tu kabla ya kufanyika mabadiliko mwaka 1995 na kujumuisha wachezaji wa mataifa yote duniani, mradi wanasakata kandanda katika vilabu vya Ulaya.
Orodha ya majina ya wachezaji 30 bora huandaliwa na baadae kupigiwa kura na wanahabari wa michezo kutoka sehemu tofauti duniani, ambapo kila nchi hupiga kura moja.
Kutoka mwaka 2010 mpaka 2015 tuzo hiyo iliunganishwa na ile ya Fifa lakini zilitengana mwaka 2016 ambapo Fifa ilianza kundaa tuzo zao wenyewe.
Washindi wa Ballon d'Or : Ronaldo & Messi watawala kuanzia 2008
2008Cristiano RonaldoLionel MessiFernando Torres
2009Lionel MessiCristiano RonaldoXavi
2010Lionel MessiAndres IniestaXavi
2011Lionel MessiCristiano RonaldoXavi
2012Lionel MessiCristiano RonaldoAndres Iniesta
2013Cristiano RonaldoLionel MessiFrank Ribery
2014Cristiano RonaldoLionel MessiManuel Neuer
2015Lionel MessiCristiano RonaldoNeymar
2016Cristiano RonaldoLionel MessiAntoine Griezmann
2017Cristiano RonaldoLionel MessiNeymar
2018Luka ModricCristiano RonaldoAntoine Griezmann
2019Lionel MessiVirgil van DijkCristiano Ronaldo

No comments:

Post a Comment