Na Deric Samora...
Sami Khedira athibitisha kuzungumza na Everton
Kiungo wa kati wa Juventus Mjerumani Sami Khedira, 33, ambaye anapanga kuhama klabu hiyo mwezi Januari, amethibitisha kuwasiliana na mkufunzi wa Everton Carlo Ancelotti. (Bild - in German)
Everton wako tayari kumpatia ofa ya uhamisho wa bila malipo kiungo wa kati Dele Alli, 24 mwezi Januari kwa lengo la kuikosesha Tottenham (Star)
Kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane amesema kuwa kiongo wa kati Mhispania Isco hayuko katika mipango yake ya siku zijazo. Hata hivyo, kiungo huyo aliye na umri wa miaka 28-anatarajiwa kuondaka klabu hiyo mwezi Januari. (Marca - in Spanish)
Mshambuliaji wa Venezuela Salomon Rondon, 31, ambaye kwa sasa anachezea klabu ya Dalian Pro, China amehusishwa na tetesi za kuhamia Wolves kushikilia nafasi ya Raul Jimenez aliyejeruhiwa. (Sun)
Paris St-Germain huenda ikamsajili mshambuliaji wa Lyon Mholanzi Memphis Depay msimu ujao lakini Barcelona wamekuwa wakimnyatia kwa muda mrefu kiongo huyo aliye na umri wa miaka 26. (Le Parisien - in French)
Tottenham wako tayari kulipa Juventus £63.6m kumunua mshambuliaji wa Argentina Paulo Dybala, 27. (TodoFichajes - in Spanish)
Tottenham wako tayari kulipa Juventus £63.6m kumnunua Paulo Dybala
Kiungo wa kati wa Lyon Mfaransa Houssem Aouar, 22, ambaye amekuwa akinyatiwa kwa muda mrefu na Arsenal, pia analengwa na Paris St-Germain huku klabu hiyo ikitarajiwa kuanza mazungumzo kumhusu mchezaji huyo hivi karibuni. (RMC - in French)
Klabu za Leeds na West Ham ni miongoni mwa Ligi ya Primia ambazo zinamsaka mlinzi wa MK Dons Matthew Sorinola,(Teamtalk)
Mazungumzo ya kuandaa pigano kati ya Anthony Joshua na Tyson Fury mwaka 2021 huenda yakachukua "siku chache" kukamilishwa, promota Eddie Hearn ameesema.
Joshua ambaye alimpiga knockout Kubrat Pulev siku ya Jumamosi imeanzisha matarajio ya mapigano kati ya wapinzani wa Uingereza.
Tetesi za Soka Jumapili
Mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe, 21, amedokeza kuwa nafasi ya yeye kuondoka Paris St-Germain itategemea ridhaa ya wazazi wake. (Copa 90, via Sun on Sunday)
Kocha wa Arsenal Mikel Arteta hajamkataa mchezaji wa Ujerumani Mesut Ozil anayechezea kikosi cha washika bunduki kabla ya mkataba wa mchezaji huyo wa miaka 32 kumalizika msimu huu. (Star on Sunday)
United tayari wamekataa mpango wa kubadilishana na Juve wakiwahusisha winga Douglas Costa, 30, na kiungo wa kati wa Barcelona Miralem Pjanic,30, ili kumnasa Pogba. (Calciomercato)
Chelsea wanajitahidi kutafuta wanunuzi wa kipa Kepa Arrizabalaga, 26, beki wa kushoto Mhispania Marcos Alonso, 29, na mlinzi wa Kidenmark Andreas Christensen, 24, ambao wote watapatikana mwezi Januari. (Sunday Express)
Kocha wa Liverpool Jurgen Klopp ameghairi chakula cha mchana wakati wa sikukuu ya Krisimasi kwa sababu ya hofu ya Covid-19. (Sunday Mirror)
No comments:
Post a Comment